24 Juni 2025 - 15:17
Qatar: Marekani imeiomba Dola kuwasiliana na Iran ili kuiomba ikubali kusitisha mashambulizi na kumaliza vita na Israel

Washington imeiomba Qatar kuwasiliana na Iran ili kujua jinsi Iran ilivyokuwa tayari kusitisha mapigano na Israel.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-Qatar imeripoti kwamba Marekani imetoa wito wa kusitisha mapigano na Iran.

Qatar: Marekani imeiomba Dola kuwasiliana na Iran ili kuiomba ikubali kusitisha mashambulizi na kumaliza vita na Israel

Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar: Rais wa Marekani Donald Trump alipiga simu na kuzungumza na Emir wa Qatar Tamim bin Hamad Al Thani baada ya shambulio la kombora la Iran kwenye kambi ya Marekani "Al-Udeid" iliyopo ndani ya Mji wa Doha - Qatar. Ilikuwa ni Washington iliyoiomba Qatar kuwasiliana na Iran na ili kujua jinsi ilivyokuwa tayari kusitisha mapigano.

Qatar: Marekani imeiomba Dola kuwasiliana na Iran ili kuiomba ikubali kusitisha mashambulizi na kumaliza vita na Israel

Kulingana na kauli ya Al-Thani, baada ya ombi la Marekani la kuiomba iwasiliane na Iran ili kuiomba kukubali kusitisha vita, Doha ilifanya mawasiliano muhimu na upande wa Iran, na hatimaye umepatikana muafaka wa makubaliano ya kusitisha mapigano.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha